Na MARGARET MAINA
Muda wa kuandaa: Dakika 20
Mapishi: Dakika 40
Walaji: 3
Biriani ni chakula kinachotengenezwa kwa wali uliokaangwa na kuchanganywa na nyama ambayo imekaangwa na masala.
Vinavyohitajika
Maelekezo
Mimina mafuta katika sufuria yapate moto kisha kaanga nyama yako iliyokwisha chemshwa mpaka iwe na rangi ya kahawia.
Ikishaiva, itoe nyama hiyo na ichuje mafuta na mafuta yanayobaki weka kitunguu na endelea kukaanga kwa dakika 10 kisha weka binzari, pilipili, giligilani, bay leaves na mbegu za hiliki.
Changanya vizuri upate mchanganyiko mzuri mkavu, halafu mwagilia yale maji ‘uliyotunza’ baada ya kuchemsha ile nyama yako
Sasa weka nyanya ndani ya sufuria yako na upike mpaka maji yakauke na mafuta yaanze kuoneka kwa juu ndani ya sufuria.
Weka nyama yako ndani ya sufuria halafu punguza moto ili ipikike kwa muda mpaka mchuzi wako na nyama viwe na ladha. Pia usisahau kuongeza chumvi kulingana na ladha unayopenda.
Chukua sufuria nyingine, mimina mafuta ya kupikia na vitunguu kisha kaanga na majani ya giligilani, majani ya mint na korosho kisha funika kwa dakika 10.
Weka mchele wako mkavu uliokwisha oshwa vizuri na uchanganye vizuri. Ongeza vikombe vitano vya maji na chumvi kiasi.
Mchele ukishaanza kuchemka, funika sufuria yako na punguza moto. Maji yakishakauka kiasi, weka mchanganyiko wa ile nyama yako nusu tu juu ya wali wa Basmati na acha wali uive kabisa.
Ni muda mchache tu halafu utakuwa tayari mlaji kupakua na kula chakula kabla hakijapoa sana.
Kikishakuwa tayari, pakua na ufurahie.