• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 7:53 PM
MAPISHI: Chipsi zilizochanganywa na nyama ya mbuzi

MAPISHI: Chipsi zilizochanganywa na nyama ya mbuzi

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 20

Muda wa kupika: Dakika 40

Walaji: 4

Vinavyohitajika

  • kilo 1 ya nyama ya mbuzi
  • ½ limau
  • vijiko 1½ vya majani ya giligilani
  • vijiko 2 vya kitunguu saumu
  • vijiko 3 cha tangawizi ya unga
  • mafuta ya kupikia
  • chumvi
  • viazi ulaya 10
  • nyanya 2
  • kitunguu maji 1
  • vijiko 2 vya nyanya ya kopo
  • pilipili 1
  • ½ kikombe vitunguu vya majani
  • kipande cha mdalasini
  • kijiko 1 cha garam masala

Maelekezo

Anza kwa kuandaa viungo kwa kukatakata majani ya giligilani, kukamua limau na vilevile kutwangatwanga kitunguu saumu.

Changanya nyama na viungo vyote kwenye bakuli kubwa.

Funika bakuli; acha viungo vikolee kwa muda wa saa kama nane au vizuri zaidi usiku kucha.

Chonga na katakata viazi vipande vidogo vya chipsi.

Weka nyanya na kitunguu katika blenda ili kutengeneza rojo; weka pembeni.

Kwenye sufuria, katika moto wa wastani, mimina mafuta mengi na yanapoanza kuchemka, weka viazi vyako viive kisha epua.

Katika kikaangio kingine, mimina mafuta na utie vitunguu.

Ongeza nyama iliyokuwa marinated. Kaanga mpaka iwe ya kahawia.

Ongeza jani la bay, rojo ya nyanya pamoja na giligilani ya unga, tangawizi na garam masala. Ongeza chumvi kisha pika mpaka nyanya ziive.

Ongeza kikombe kimoja cha maji. Funika na acha nyama iive kwa moto wa chini kwa muda wa nusu saa.

Ongeza viazi kwenye nyama na sosi vichanganye kabla ya kuepua.

Kisha pakua na ufurahie.

You can share this post!

Familia kadhaa zafurushwa kutoka kipande cha ardhi...

Simba waliolemewa na njaa wapata ufadhili wa chakula

adminleo