• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 9:50 AM
MAPISHI: Jinsi ya kupika maini ya ng’ombe

MAPISHI: Jinsi ya kupika maini ya ng’ombe

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 10

Muda wa kupika: Dakika 20

Walaji: 3

Maini ambayo hayajapikwa. Picha/ Margaret Maina

Vinavyohitajika

maini ya ng’ombe kilo 1

nyanya 4

kitunguu maji 1

karoti 1

pilipili mboga za rangi tofauti

juisi ya limau vijiko 3

chumvi

majani ya giligilani

mafuta ya kupikia

Utaratibu

Anza kwa kutayarisha maini. Ondoa ngozi ya juu ya ini ambayo huwa ngumu.

Osha kisha kata vipande kwenye ukubwa unaopenda.

Nyunyuzia juisi ya limau kwenye vipande vya ini na kisha weka chumvi.

Changanya vizuri ili vipande vichanganyike sawia.

Andaa viungo kwa kuosha na kuvikata vipande vidogo; nyanya, pilipili mboga, karoti na vitunguu.

Weka mafuta ya kupikia kwenye sufuria, au kikaangio unachotumia kupikia maini.

Weka maini. Yakaange hadi yaive kama dakika 10.

Weka kitunguu, koroga na uache viive vizuri.

Weka pilipili mboga na karoti. Koroga kwa dakika tano.

Weka nyanya huku ukikoroga; punguza moto uwe wa wastani.

Baada ya dakika 10 unaweza kuepua kwa kuwa nyama imeiva.

Nyama ya maini ambayo imeiva. Picha/ Margaret Maina

Pakua kwa wali,chapati,viazi vilivyobondwa au chochote ukipendacho na ufurahie

You can share this post!

Serikali kupimia wazee hewa

SIHA NA LISHE: Mnywaji wa chai yenye tangawizi anapata...

adminleo