• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 10:48 AM
PATA USHAURI: Fahamu ugonjwa wa homa ya ini

PATA USHAURI: Fahamu ugonjwa wa homa ya ini

Na PAULINE ONGAJI

HOMA ya ini au Hepatitis B ni ugonjwa wa kuambukizwa unaotokana na virusi vya Hepatitis B Virus (HBV).

Japo maambukizi haya ni hatari sana na yaweza kusababisha kifo endapo hayatatibiwa, yaweza kuzuiwa kwa kutumia chanjo.

Unavyoambukizwa

• Kujamiana bila kinga

• Kupigana denda

• Kuchangia damu isiyo salama

• Kuchangia sindano, wembe, miswaki, au hata taulo

• Mama mwenye ugonjwa kumwambukiza mtoto wakati wa kujifungua

Lazima mgonjwa akaguliwe na mtaalamu wa kimatibabu ambapo mara nyingi uchunguzi kwenye maabara huhitajika.

Ishara

• Uchovu na mwili kuwa dhaifu

• Kichefuchefu

• Homa kali

• Kupoteza hamu ya kula na kupungua uzito.

• Maumivu makali ya tumbo upande wa ini

• Macho na ngozi kuwa manjano

• Mkojo mweusi au wa utusiutusi

Kwa waathiriwa wengi, hali huwa mbaya zaidi na kusababisha saratani ya ini.

Kinga

• Chanjo

• Kutumia kinga wakati wa kujamiiana

• Kuacha kuchangia sindano, wembe, miswaki au hata taulo

Unashauriwa kutumia vyakula vinavyosaidia kuua bakteria na virusi hasa vyenye kuongeza kinga mwilini kama vile matunda na mboga.

You can share this post!

PATA USHAURI: Athari za maziwa ya poda na yale ya ng’ombe...

PATA USHAURI WA DKT FLO: Jipu kubwa sehemu nyeti chungu sana

adminleo