Shangazi Akujibu

SHANGAZI AKUJIBU: Anadai wanaongea na ex kuhusu watoto, hii ni kweli au nitakuja kujuta

Na SHANGAZI November 15th, 2025 Kusoma ni dakika: 1

SWALI: Hujambo shangazi. Nilimpata mume wangu akiongea kwa sauti ya chini na ex wake usiku. Alisema alikuwa anamuuliza jinsi watoto wanavyoendelea. Je, hii ni ishara ya usaliti?

Jibu: Sielewi kwa nini huyo waliyeachana apige simu usiku. Hii ni ishara unayostahili kuifuatilia kwa makini na kuweka mipaka mapema kuhusu heshima na kinachostahili kufanyika.

IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO