Shangazi Akujibu

SHANGAZI AKUJIBU: Anang’ang’ania eti tuishi pamoja na mama mkwe!

Na SHANGAZI December 9th, 2025 Kusoma ni dakika: 1

SWALI: Za kwako shangazi. Mpenzi wangu anataka tukae na mama yake baada ya harusi. Mimi sitaki sababu najua tabu za mama mkwe. Nifanyeje?

Jibu: Hili ni jambo kubwa linalohitaji mazungumzo ya wazi kabla ya ndoa. Elezea kwa heshima lakini kwa uthabiti kwamba unahitaji nafasi yenu binafsi baada ya harusi.

IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO