Shangazi Akujibu

SHANGAZI AKUJIBU: Mke wangu anapuuza majukumu ya nyumbani sababu ya biashara

Na SHANGAZI October 31st, 2025 Kusoma ni dakika: 1

SWALI: Tangu mke wangu aanze biashara, hanipi tena muda. Ameniachia majukumu yote ya nyumbani. Nikizungumza naye anasema simwelewi. Nifanye nini?

 

JIBU: Ndugu, dunia imebadilika—wanawake nao wanakimbizana na kazi na biashara kama wanaume. Usimlaumu moja kwa moja, bali tafuteni njia ya kuhakikisha kuwa hakuna anayevunjwa na majukumu ya nyumbani. Msaidiye pale inapoweza, kisha muweke ratiba. Ndoa si mashindano ya nani anafanya zaidi, bali ushirikiano.

IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO