Shangazi Akujibu

SHANGAZI AKUJIBU: Mpenzi amehepa baada ya kunipachika mimba

Na SHANGAZI December 7th, 2025 Kusoma ni dakika: 1

SWALI: Tangu mpenzi wangu anipachike mimba, amejitenga sana. Hashiki simu zangu wala kujibu SMS ninazomtumia. Sijui nifanye nini.

Jibu: Kujitenga kwake baada ya mimba ni dalili ya kutowajibika. Jaribu mazungumzo ya moja kwa moja ili kupata msimamo wake. Akikwepa bado, anza kuangalia maisha yako na ya mtoto wako.

IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO