Shangazi Akujibu

SHANGAZI AKUJIBU: Mpenzi anaugua lakini hataki kwenda hospitalini, nifanyeje?

Na SHANGAZI November 27th, 2025 Kusoma ni dakika: 1

SWALI: Vipi Shangazi. Binti ninayempenda anaonekana mgonjwa, kikohozi, homa, ana tatizo la kupumua. Lakini hataki twende hospitalini. Anasema yeye ni buheri wa afya. Nisaidie.

Jibu: Penzi si dawa. Kama hana nia ya kutunza afya yake, atawezaje kutunza mapenzi yenu? Akikataa jua kuna jambo analoficha.

IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO