Shangazi Akujibu
SHANGAZI AKUJIBU: Mume wangu ametoweka na msichana wetu wa kazi!
Mjakazi akisafisha huku mwanaume akiwa ameketi akisoma gazeti. Picha|Maktaba.
SWALI: Shikamoo shangazi. Nina mume na watoto wawili. Mwezi uliopita mume wangu alitoweka na mfanyakazi wetu wa nyumbani. Baadaye alinipigia simu akaniambia huyo sasa ndiye mke wake. Ameahidi kugharamia mahitaji yetu. Nishauri.
Jibu: Uhusiano wa kimapenzi na ndoa hutokana na hiari. Iwapo mume wako ameamua hataki ndoa kati yenu, huwezi kumlazimisha. Kubali uamuzi huo na uendelee na maisha yako.
IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO