Shangazi Akujibu

SHANGAZI AKUJIBU: Mwanangu ameanza kuiba vifaa vidogo vidogo kwa nyumba na akana peupe

Na SHANGAZI December 22nd, 2025 Kusoma ni dakika: 1

SWALI: Nimegundua mwanangu anaiba vifaa vidogo pale nyumbani. Kwa mfano, alichukua simu ya nyumbani akauza. Nilipomuuliza alikana kabisa kutoweka kwa kifaa hicho. Chakula kikibaki pia anaiba. Nifanyeje?

Jibu: Ni mapema sana kumuita mwizi. Chunguza chanzo cha tabia hiyo kwanza kisha rekebisha tabia yake mapema kwa mazungumzo na nidhamu ya upendo.

IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO