Shangazi Akujibu

SHANGAZI AKUJIBU: Nashuku ataniacha sababu sijamzalia

Na SHANGAZI February 3rd, 2026 Kusoma ni dakika: 1

SWALI:  Salamu Shangazi. Nimekuwa katika ndoa kwa miaka mitatu. Tatizo ni kuwa nimeshindwa kabisa kupata mtoto. Mume wangu anapenda watoto sana na nahofia ataniacha. Nifanyeje?

Jibu: Kumekuwa na dhana potovu kuwa shida ya kutopata watoto ni ya wanawake pekee. Wanaume pia huwa na shida hiyo. Kama hamjapimwa hospitalini ni muhimu mfanye hivyo ili mjue kiini cha tatizo hilo na iwapo linaweza kutibiwa.

IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO