Shangazi Akujibu
SHANGAZI AKUJIBU: Nashuku mke wangu ana mpenzi mwingine
Wanandoa wanaofarakana kwa sababu ya mchezo wa huba. Picha|Maktaba
SWALI: Mambo shangazi? Nimeoa na nampenda sana mke wangu. Lakini nashuku ana mpango wa kando kwani tabia yake imebadilika sana. Ameanza kuchelewa sana kazini na mara nyingi anasusia huduma za chumbani akidai amechoka. Nina wasiwasi.
Jibu: Hizo ni dalili za kutia hofu. Inawezekana mwenzako anaonana na mwanamume mwingine. Lakini huwezi kumuuliza kwa sababu huna ushahidi. Makinika kuchunguza mienendo yake. Iwapo ana mwingine utawafumania ndipo ufanye uamuzi unaofaa.
IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO