Shangazi Akujibu
SHANGAZI AKUJIBU: Nimepata biashara ya kuzalia mtu, sitaki mume ajue
Mwanamke mjamzito. Picha|Maktaba
SWALI: Shikamoo shangazi. Nimepata biashara ya ‘kuzaa’. Yaani unalipwa vizuri kubeba mimba na sitaki mume wangu ajue. Nifanyeje?
Jibu: Dada, kubeba mimba kwa sababu ya pesa si jambo la mchezo. Kama huna ujasiri kumwambia, basi hiyo biashara si ya heshima kwako wala kwa ndoa yako.
IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO