Shangazi Akujibu

SHANGAZI AKUJIBU: Ninayemmezea mate anampenda rafiki yangu

Na SHANGAZI November 3rd, 2025 Kusoma ni dakika: 1

SWALI: Hujambo shangazi. Nimegundua kuwa mwanaume ninayemmezea mate anampenda rafiki yangu. Hii imenifanya nipoteze matumaini na masuala ya mapenzi. Naomba unipe ushauri wako ushauri.

Jibu: Usihuzunike. Wakati mwingine maisha hutukumbusha kuwa si kila tunayetaka atatutaka. Huyo mwanaume si wa mwisho duniani. Jipende, na ufahamu kuwa anayekufaa yupo njiani.

IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO