Shangazi Akujibu
SHANGAZI AKUJIBU: Rafiki yangu asema mpenzi wangu anamkatia, nifanyeje?
Wapenzi wakionyeshana malavidavi.Picha|Hisani
SWALI: Za kwako shangazi. Rafiki yangu ameniambia eti mpenzi wangu amekuwa akitaka wawe na mpango wa kando kwa sababu simtoshelezi kimapenzi. Habari hizo zimenichoma vibaya moyoni. Nifanyeje?
Jibu: Hakuna mwanamume anayependa kuhusishwa na upungufu wa aina hiyo. Mpenzi wako aliona aibu kukwambia na alijua utaumia moyoni. Sasa umejua. Shauriana naye kuhusu mwelekeo wa uhusiano wenu.
IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO