Shangazi Akujibu
SHANGAZI AKUJIBU: Tulikosana na mpenzi wangu tukaachana, sasa anataka turudiane
Wanandoa wanaofarakana. Picha| Maktaba.
SWALI: Kwako shangazi. Mapema mwaka huu nilikosana kidogo na mwanamke mpenzi wangu na tukaachana. Juzi alinitumia ujumbe akiniomba tuwe marafiki. Mimi nataka mapenzi si urafiki. Waonaje?
Jibu: Mapenzi huanza kwa urafiki na wahusika wanaweza kuendelea na urafiki hata wakiachana. Inawezekana mwanamke huyo anatafuta jinsi ya kufufua uhusiano wenu. Ukikubali utapata nafasi ya kumshawishi mrudiane.
IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO