• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 8:50 AM
SIHA NA LISHE: Faida ya kula mapera

SIHA NA LISHE: Faida ya kula mapera

Na MARGARET MAINA

[email protected]

MAPERA ni matunda baadhi ya watu husema yana ugumu wakiyala.

Hata hivyo, yakishaiva huwa laini. Muhimu ni kwamba huwa yana nyama na mbegu mbegu nyingi.

Matunda haya yana faida kubwa sana kwa afya ya mwili wa mwanadamu jinsi ifuatavyo: –

Yana vitamini C

Mapera yana ukwasi mkubwa wa Vitamini C ambayo ni muhimu sana katika mwili wa mwanadamu.

Ni kinga nzuri ya kisukari

Ulaji mbaya wa watu wengi unawaweka katika hatari ya kuugua kisukari.

Mapera yatakupunguzia hatari ya kupatwa na ugonjwa wa kisukari.

Hii ni kwa sababu mapera yana utajiri mkubwa sana wa nyuzinyuzi (fibre), ambayo ni muhimu sana katika kupunguza kiasi cha sukari kwenye damu.

Mapera. Picha/ Margaret Maina

Kuimarisha uwezo wa kuona

Mapera yana utajiri mkubwa sana wa vitamini A au Retinol ambayo ni muhimu sana katika kusaidia kuona vizuri. Hivyo basi kama ilivyo kwa karoti, mapera yanasaidia katika kuongeza na kuimarisha uwezo wa mtu kuona.

Kurekebisha kiwango cha shinikizo la damu

Madini ya Potassiumu yaliyomo ndani ya mapera yanasaidia katika kurekebisha shinikizo la damu (Blood Pressure).

Yana madini ya shaba

Mapera yana madini ya shaba (Trace element copper ) ambayo ni mazuri sana katika ufanyaji kazi wa thyroid.

Tezi za thyroid zisipofanya kazi vizuri zinaweza kusababisha matatizo mengi ya kiafya kwa mwanadamu.

Yana madini ya manganese

Mapera yana utajiri mkubwa wa madini ya manganese ambayo yanausaidia mwili katika kunyonya ama kupata virutubisho muhimu kutoka kwenye vyakula tunavyo kula.

Mapera ni muhimu katika afya ya akili ya mwanadamu

Vitamini B3, Vitamini B6 ambazo zinapatikana ndani ya tunda la mpera ni muhimu katika kuimarisha afya ya akili ya mwanadamu. Mapera yatasaidia kuufanya ubongo wako utulie.

Ni muhimu sana katika ngozi ya mwanadamu

Vitamini C, viondoa sumu na karotini ambazo zinapatikana ndani ya tunda la mpera ni muhimu sana katika kuimarisha afya ya ngozi.

You can share this post!

Dani Alves ahusishwa na uhamisho kujiunga na Arsenal

SIHA NA LISHE: Viungo mbalimbali na faida katika mapishi na...

adminleo