Na MARY WANGARI
HAYA ni matamshi ya mzungumzaji yanayojitokeza kutokana na athari za lugha yake ya kwanza; lugha inayotumika katika mazingira anamoishi au maumbile katika ala za sauti.
Aidha, tunaweza kufafanua lafudhi kuwa ni upekee unaojitokeza kwa mtu binafsi na huleta tofauti baina ya wasemaji au jamii.
Lugha ishara
Hii ni lugha ya mawasiliano inayotumia ishara badala ya sauti na maneno.
Lahaja (Dialect)
Hii ni tofauti katika matamshi, maumbo na matumizi ya maneno zitokanazo na tofauti katika maeneo mbalimbali kwa lugha yenye asili moja.
Lahaja inaposanifishwa hupata hadhi ya kuwa lugha.
Hakuna makubaliano kamili kuhusu idadi ya lahaja za Kiswahili na mipaka yake. Hii ni kwa sababu uchunguzi kamili haujafanywa.
Asili ya lahaja tofauti ndogondogo katika lugha hutegemea maeneo mbaimbali na hutokea katika vipengele vifuatavyo:
Matumizi na manufaa ya lahaja
Ijapokuwa lahaja kwa kiwango fulani hutatiza mawasiliano, zina umuhimu wake jinsi tutakavyoainisha ifuatavyo:
Hutumiwa katika kukuza lugha kwa kupanua msamiati wake. Kwa mfano, maneno kama vile rununu, kipakatalishi, tovuti na kadhalika.
Hutumiwa katika kusanifisha lugha.
Hudhihirisha utajiri wa lugha kupitia mitindo mbalimbali ya wazungumzaji.
Hunogeza lugha kwa kutia ladha mazungumzo ya wasemaji mbalimbali.
Huwakilisha historia ya lugha.
Hudhihirisha ukwasi wa lugha
Kuna lahaja mbalimbali za Kiswahili ambazo huainishwa kulingana na eneo la kijiografia zinakozungumzwa.
Marejeo
Chiraghdin, S., Mnyampala, M. (1977). Historia ya Kiswahili. Nairobi: Oxford University Press.
Richards, J.C., (1984). Error Analysis Perspectives on Second Language Acquisition. London: Longman Group Ltd.
Wardhaugh, R. (1986). An Introduction to Socio-Linguistics. New York: Blackwell Publishers