Na MARGARET MAINA
VIAZI kwa kawaida ni chakula chenye madini mengi muhimu kama vitamini A, C, B, na iron.
Viazi vina manufaa kwa ngozi zetu waja.
Unaweza kutumia viazi nyumbani ili kuifanya ngozi iwe nyororo.
Faida za viazi kwa ngozi
Viazi huondoa madhara ambayo yanakuwa yamesababishwa na jua na kuleta mwanga wa asili wa ngozi.
Viazi vinapunguza wekundu na matatizo ya ngozi kutokana na vipele ,makovu na chunusi.
Viazi vinafanya ngozi iwe ya rangi moja na laini.
Viazi husaidia kuondoa mikunjo kwenye uso.
Viazi huondoa weusi kwenye kwapa.
Ili kusaidia ngozi iwe na rangi moja
Utahitaji
Cha kufanya
Kwenye kijibakuli changanya mahitaji au hivi vyote vinavyohitajika na upake kwenye uso bila ya kusahau shingo na sehemu zote utazohitaji.
Ache kwa muda wa nusu saa kisha osha kwa maji fufutende.
Kuondoa makovu na madoa
Unahitaji
Cha kufanya
Nyunyiza sukari kidogo kwenye kipande cha kiazi na ujisugue kwa dakika tano.
Uache mchanganyiko kwenye uso wako kwa dakika kumi, kisha osha kwa maji baridi.
Kuondoa weusi na madoa
Limau na viazi hutumika kama mkorogo wa asili na huondoa weusi wowote na madoa kwenye ngozi.
Unahitaji
Cha kufanya
Ponda kiazi na weka vijiko vitatu vya juisi ya limau.
Changanya na paka kwenye makovu.
Iache kama dakika 20 mpaka 30 kisha osha vizuri na maji.
Kwa ngozi iliyoungua na jua
Maji ya viazi yatasaidia ngozi yako
Unahitaji
Cha kufanya
Changanya hivi vyote vinavyohitajika pamoja na upake kwenye uso.
Acha kama dakika 15 kisha osha.
Kausha vizuri na paka losheni au mafuta unayopenda.
Kuondoa mikunjo
Viazi huondoa na kupunguza mikunjo kwenye uso.
Unahitaji
Cha kufanya
Katika bakuli, tia kiazi kilichopondwa na maziwa, changanya vizuri.
Ongeza gycrerine na changanya.
Paka mchanganyiko kwenye uso wako na uache kama dakika 15.
Osha kwa maji fufutende kisha ufute uso kwa taulo safi.