• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:15 PM
Dereva Jim Heather-Hayes atawazwa mwanamichezo bora mbio za magari baada ya kufariki  

Dereva Jim Heather-Hayes atawazwa mwanamichezo bora mbio za magari baada ya kufariki  

NA GEOFFREY ANENE

MWENDAZAKE Jim Heather-Hayes ametawazwa mwanamichezo bora wa mwaka 2023 wa Shirikisho la Mbio za Magari nchini Kenya (KMSF).

Heather-Hayes alikuwa dereva maarufu katika mbio za magari enzi zake.

Alifariki mwaka 2022 na alikuwa mmoja wa madereva waliovuma katika mashindano ya magari na ametambuliwa kwa mchango wake wa muda mrefu katika mchezo huo.

Heather-Hayes alichangia pakubwa katika kulea mabingwa wa siku zijazo.

Matokeo yake mazuri kabisa katika mbio za magari za Safari Rally yalipatikana mwaka 1990 alipomaliza nambari sita kwa jumla.

Heather-Hayes alishiriki Safari Rally kwa mara ya kwanza ikiwa duru ya Mbio za Magari Duniani (WRC) mwaka 1984 ikidhaminiwa na Marlboro.

Mwenyekiti wa KMSF, Maina Muturi alivulia kofia Heather-Hayes akisema kutuzwa kwake ni ushahidi tosha wa kujitolea kwake na bidii pamoja na ari yake katika michezo ya magari kwa miaka mingi.

Bw Maina aliongeza kuwa Heather-Hayes alionyesha kujitolea katika mchezo huo na kumfanya mtu aliyestahili tuzo hiyo iliyoanzishwa miaka ya 1960.

Hafla hiyo ya KMSF ya kuwapa zawadi wanamichezo waliong’aa katika michezo ya magari hufanyika kila mwaka.

Waziri wa Michezo na Masuala ya Vijana, Bw Ababu Namwamba na Katibu, Peter Tum pia walimpa zawadi mfalme wa mbio za magari za Afrika Karan Patel na bingwa wa mbio za magari za Afrika za chipukizi Hamza Anwar.

Miongoni mwa mabingwa wa msimu 2023 waliozawadiwa kwa sababu ya kazi nzuri ni ndugu Jasmeet Chana na Ravi Chana walioshinda Mbio za Magari za Kitaifa nchini Kenya (KNRC) na pia kitengo cha B13.

Jasmeet ni mmoja wa madereva wachache ambao wameshinda karibu kila kitengo katika mbio za magari nchini, ikiwemo Kundi N, Madaraja ya Kwanza na Tatu na 2WD katika miaka yake ya kwanza katika fani hii.

Tim Jessop, ambaye alielekeza dereva Carl Tundo kunyakua mataji matano ya duru ya Afrika ya Safari Rally, alituzwa mshindi wa jumla wa mbio za kitaifa za Rally Raid.

Ndugu Chantal na Zane Young waliibuka washindi wa kitengo cha vigari cha Rally Raid.

Nyota anayeinuka kwa haraka Neel Gohil alitunukiwa zawadi ya kutwaa ubingwa wa mbio za vigari za kitaifa za Autocross.

Eric Bengi, John Kadivani na Azaad Manji walishinda Autocross katika vitengo vya magari ya 4WD-T, wazi na 2WD-T.

Namwamba, ambaye alikuwa mgeni wa heshima, aliahidi kuimarisha hadhi ya KNRC na fani mbalimbali za magari ili kuhakikisha kuwa Wakenya wanajiandaa vyema kwa duru ya dunia ya Safari Rally.

“Hatuwezi kujisifu kuwa na mashindano magumu na yanayofahamika kote duniani ya WRC halafu ligi ya hapa nyumbani haina nguvu. Ningependa kuomba wadhamini na wahisani kushirikiana nasi ili kuhakikisha tunapata ubora tuliokuwa nao katika mbio za magari miaka ya nyuma,” alisema Bw Namwamba.

Hafla ya kutuza wanamichezo wa mbio za magari iliandaliwa katika hoteli ya kifahari ya Carnivore jijini Nairobi na kuhudhuriwa na wageni kutoka nje ya Kenya, wakiwemo marais wa mbio za magari Christian Gakwaya (Rwanda) na Dipu Ruparelia (Uganda).

WASHINDI WA TUZO ZA KMSF MWAKA 2023:

Rally Raid

Bingwa wa Rally Raid – Tim Jessop

Dereva bora wa Rally Raid – Alasdair Keith

Mwelekezi bora wa Rally Raid – Charles Mousley

Dereva bora wa kitengo cha Prototype – Mark Glen

Mwelekezi bora wa kitengo cha Prototype – Douglas Rundgren

Dereva bora wa kitengo cha Modified – Alasdair Keith

Mwelekezi bora wa kitengo cha Modified – Charles Mousley

Dereva bora wa vigari vya Buggy – Zane Young

Mwelekzi bora wa vigari vya – Chantal Young

Tarmac

Kitengo cha 4WD – Leroy Mwamba

Kitengo cha 2WD – Moses Mwendwa

Karting

Kitengo cha Bambino – Wilf Mulyanga

Kitengo cha kadeti – Bixente Rio Wyles

Kitengo cha Rotax Junior Max – Krrish Vadgama

4 x 4 

Dereva mwanafunzi – Gabriel Lauvaux/Mwelekezi mwanafunzi – Olivier Lauvaux

Dereva wasta – Ben Waiyaki/mwelekezi wasta – Prabjot Saimbi

Dereva stadi – Gurashish Singh/ mwelekezi stadi – Kunal Patel

Dereva stadi kabisa – Oliver Lauvaux/mwelekezi stadi kabisa – John Herbert

Autocross

Kitengo cha Kwanza – 2wd Non-Turbo Buggy: Neel Gohil

Kitengo cha Pili – 2wd Non-Turbo Car: Neel Gohil

Kitengo cha Tatu – 2wd Turbo Buggy: Azaad Manji

Kitengo cha Nne – 4wd Non-Turbo: Jose Sardinha

Kitengo cha Tano – 4wd Turbo: Eric Bengi

Kitengo cha Sita – Open: John Kadivane

Kitengo cha Nane – Bambino: Eann Bengi

Kitengo cha Tisa – Junior 2wd Non-Turbo: Karamveer Singh Roopra

Kitengo cha 10 – Peewee: Allan Bengi

Washindi wa Mbio za Magari za Afrika (ARC)

Dereva: Karan Patel/Mwelekezi: Tauseef Khan

Washindi wa KNRC

Classic: Dereva Ian Duncan/mwelekezi: Jaspal Matharu

2wd: Dereva Daren Miranda/mwelekezi: Linet Ayuko

SPV: Dereva Jose Sardinha/mwelekezi Shameer Yusuf

S: Dereva Kush Patel/mwelekezi: Mudasar Chaudry

Rally Raid: Dereva Chinu Matharu/mwelekezi: Raju Chaggar

B13: Dereva Jasmeet Chana/mwelekezi: Ravi Chana

N: Dereva Nikhil Sachania/mwelekezi: Deep Patel

Rally 3: Dereva McRae Kimathi/mwelekezi: Mwangi Kioni

Rally 2: Dereva Samman Vohra/mwelekezi: Alfir Khan

Mabingwa wa jumla wa KNRC: Dereva Jasmeet Chana/mwelekezi: Ravi Chana

 

  • Tags

You can share this post!

Passaris awapuuza waliomzomea wakati wa maandamano kukemea...

Arati na Osoro watumiwa kamishna mpya kupambana na vurugu...

T L