• Nairobi
  • Last Updated April 30th, 2024 8:55 PM
GOLD COAST AUSTRALIA: Matokeo ya aibu kwa Kenya mita 400 kuruka viunzi

GOLD COAST AUSTRALIA: Matokeo ya aibu kwa Kenya mita 400 kuruka viunzi

Na GEOFFREY ANENE

PACHA Nicholas Bett na Aron Koech wameambulia pakavu katika mbio za mita 400 za kuruka viunzi kwenye Michezo ya Jumuiya ya Madola mjini Gold Coast, Australia, Alhamisi.

Bingwa wa dunia mwaka 2015, Bett, alivuta mkia baada ya kukamilisha umbali huo kwa sekunde 51.00. Licha ya kutopata matokeo mazuri tangu ufanisi huo wake jijini Beijing nchini Uchina miaka mitatu iliyopita, Bett alikuwa amepigiwa upatu kushindia Kenya medali.

Alikosa Riadha za Dunia za mwaka 2017 jijini London, Uingereza, kutokana na jeraha. Koech alikuwa jijini London, lakini hakufanya vyema. Aliondolewa mashindanoni katika nusu-fainali.

Mjini Gold Coast, Koech alimaliza katika nafasi ya sita kwa sekunde 50.02. Kyron McMaster kutoka Visiwa vya British Virgin, ambaye mwaka 2017 aliondolewa mashindanoni kwa kuvunja sheria za kutobadilisha laini jijini London, ametwaa ubingwa kwa sekunde 48.25.

Jeffery Gibson, ambaye alimaliza Riadha za Dunia katika nafasi ya tatu mwaka 2015, amenyakua nishani ya fedha kwa sekunde 49.10 naye Mjamaica Jaheel Hyde akaridhika na shaba kwa sekunde 49.16.

You can share this post!

Kocha mpya wa Simbas atambulishwa

Makarani kuwasilisha mswada bungeni kulinda maslahi yao

adminleo