• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 5:20 PM
Joylove sare, mabinti wa Mukuru warudi Nairobi kwa raha

Joylove sare, mabinti wa Mukuru warudi Nairobi kwa raha

Na JOHN KIMWERE

TIMU ya wanawake ya Sunderland Samba ilijikuta njia panda mbele ya Joylove FC huku Mukuru Talent Queens ikicharaza Moving The Goalposts (MTG) United kwa mabao 3-2 kwenye mechi ya Soka kuwania Ligi ya Taifa Daraja ya Kwanza iliyopigwa mjini Mombasa.

Mukuru Talent Queens ya kocha Amos Abong’o ilirejea jijini Nairobi kwa tabasamu baada ya kuvuna alama tatu ugenini kwenye utangulizi wa kampeni zake msimu huu.

Mchezo huo haukuwa mteremko na vigoli hao walipata shughuli zito mbele ya wenyeji wao waliokuwa wakishabikiwa na wafuasi wa nyumbani.

Kocha Joyce Akinyi wa Joylove FC akiwapa ushauri wachezaji wake kabla ya kuingia mzigoni kukabili Sunderland Samba kwenye mechi ya Ligi ya Taifa Daraja ya Kwanza uwanjani KNH, Nairobi. Picha/ John Kimwere

Mukuru Talent ikiongozwa na nahodha, Belinda Awour ilitwaa ushindi huo kupitia jitihada zao Amina Musindi, Carolyne Simiyu na Shangila Ramadhan waliotinga bao moja kila mmoja.

”Tumeanza michezo yetu vizuri licha ya kuzoa ushindi mwepesi,” kocha wa Mukuru Talent Queens alisema.

Sunderland Samba ilitoka chini mabao 2-0 na kujituma kiume kabla ya kukubali kutoka sare ya magoli 3-3 dhidi ya Joylove ilionekena kuja kivingine msimu huu.

Wafungaji wa Sunderland Samba walikuwa Irene Aluoch, Sylvia Akoth na Elizabeth Majuma waliopiga moja safi kila mmoja.

Kwa Joylove FC Faith Evayo alitingia mabao mawili huku Pesah Naliaka akicheka na wavu mara moja. Nayo Limuru Starlets ililala kwa mabao 2-1 na Soccer Sisters.

You can share this post!

Ni kivumbi fainali za Chapa Dimba Kaskazini Mashariki

Wazito warejea kileleni, Ushuru yateleza

adminleo