• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 8:55 PM
Macho kwa Mbwana Samatta na Mohamed Salah huku Tanzania na Misri zikipimana nguvu

Macho kwa Mbwana Samatta na Mohamed Salah huku Tanzania na Misri zikipimana nguvu

Na GEOFFREY ANENE

TAIFA Stars ya Tanzania inatarajia kuwa na mechi nzuri inapimana nguvu dhidi ya wenyeji wa Kombe la Afrika (AFCON) 2019 Misri uwanjani Borg El Arab mjini Alexandria leo Alhamisi saa nne usiku.

Shirikisho la Soka nchini Tanzania (TFF) limenukuu Kocha wa viungo Abdelrahman Essa akisema mechi hiyo ya kwanza kirafiki ni muhimu sana kwa Taifa Stars ambayo itakutana na Senegal, Kenya na Algeria katika mechi za Kundi C kwenye AFCON jijini Cairo mnamo Juni 23, Juni 27 na Julai 1 mtawalia.

“Natarajia mechi hiyo iwe ya kufana,” ameongeza raia wa Misri, Essa, ambaye aliajiriwa katika benchi la kiufundi la Tanzania hapo Juni 11.

Kipa Aishi Manula kutoka Simba SC amesema Tanzania itakuwa ikitafuta matokeo mazuri dhidi ya Wamisri, ambao wanajivunia mataji mengi ya AFCON kuliko taifa lingine lolote barani Afrika (saba). “Misri ni kipimo tosha. Mechi hii itatupa nafasi ya kuonyesha kile tumejifunza. Ni mechi ambayo tunataka kupata matokeo mazuri….”

Tanzania haijawahi kupata sare ama kushinda Misri katika mechi tano mataifa haya yamekutana kati ya mwaka 1980, ambayo ni mara ya mwisho Taifa Stars ilikuwa AFCON, na mwaka 2016 zilipokutana mara ya mwisho. Kwa jumla, Misri imefunga Tanzania mabao 17-3 katika mechi hizo. Macho yatakuwa kwa nyota wa Tanzania, Mbwana Samatta, ambaye aliibuka mfungaji bora katika Ligi Kuu ya Ubelgiji msimu 2018-2019, na Mohamed Salah, ambaye kwa msimu wa pili mfululizo alinyakua tuzo ya mfungaji bora kwenye Ligi Kuu ya Uingereza. Misri iko katika Kundi A pamoja na DR Congo, Uganda na Zimbabwe. Mataifa 24 yatashiriki AFCON mwaka 2019.

VIKOSI VYA KUNDI ‘C’

Kundi A

Senegal (namba moja Afrika & 23 duniani)

Makipa – Abdoulaye Diallo (Rennes, Ufaransa), Alfred Gomis (Spal, Italia), Edouard Mendy (Reims, Ufaransa); Mabeki – Kalidou Koulibaly (Napoli, Italia), Moussa Wague (Barcelona, Uhispania), Pape Abdou Cisse (Olympiacos, Ugiriki), Salif Sane (Schalke,Ujerumani), Youssouf Sabaly (Bordeaux, Ufaransa), Lamine Gassama (Goztepe, Uturuki), Saliou Ciss (Valenciennes, Ufaransa), Cheikhou Kouyate (Crystal Palace, Uingereza); Viungo – Alfred Ndiaye (Malaga, Uhispania), Idrissa Gana Gueye (Everton, Uingereza), Keprin Diatta (Club Brugge, Ubelgiji), Pape Alioune Ndiaye (Galatasaray, Uturuki), Henri Saivet (Bursaspor, Uturuki); Washambuliaji – Ismaila Sarr (Rennes, Ufaransa), Keita Balde (Inter Milan, Italia), Mbaye Niang (Rennes, Ufaransa), Moussa Konate (Amiens, Ufaransa), Mbaye Diagne (Galatasaray, Uturuki), Sada Thioub (Nimes, ufaransa), Sadio Mane (Liverpool, Uingereza)

Algeria (nambari 13 Afrika & 70 duniani)

Makipa – Rais M’Bolhi (El Etifaq, Saudi Arabia), Azzedine Doukha (Al Raed, Saudi Arabia), Alexandre Oukidja (Metz, Ufaransa); Mabeki – Aissa Mandi (Real Betis, Uhispania), Mehdi Zeffane (Rennes, Ufaransa), Ramy Bensebaini (Rennes, Ufaransa), Rafik Halliche (Moreirense, Ureno), Mehdi Tahrat (Lens, Ufaransa), Djamel Benlamri (Al Shabab, Saudi Arabia), Youcef Atal (Nice, Ufaransa), Mohamed Fares (Spal, Italia); Viungo – Mohamed Benkhemassa (USM Alger, Algeria), Ismail Bennacer (Empoli, Italia), Mehdi Abeid (Dijon, Ufaransa), Sofiane Feghouli (Galatasary, Uturuki), Adlene Guedioura (Nottingham, Uingereza), Hicham Boudaoui (Paradou, Algeria); Washambuliaji – Adam Ounas (Naples, Italia), Riyad Mahrez (Manchester City, Uingereza), Islam Slimani (Fenerbahce, Uturuki), Yacine Brahimi (Porto, Ureno), Baghdad Bounedjah (Al Sadd, Qatar), Youcef Belaili (Esperance Tunis, Tunisia)

Kenya (nambari 25 Afrika & 108 duniani)

Makipa – Patrick Matasi (St Georges, Ethiopia), John Oyemba (Kariobangi Sharks), Farouk Shikalo (Bandari); Mabeki – Abud Omar (Sepsi Sf. Gheorghe, Romania), Joash Onyango (Gor Mahia), Joseph Okumu (Real Monarchs, Marekani), Musa Mohammed (Nkana, Zambia), David Owino (Zesco United, Zambia), Bernard Ochieng (Vihiga United), Brian Mandela (Maritzburg, Afrika Kusini), Philemon Otieno (Gor Mahia), Erick Ouma (Vasalund, Uswidi); Viungo – Victor Wanyama (Tottenham Hotspur, Uingereza), Anthony Akumu (Zesco United, Zambia), Ismael Gonzalez (Las Palmas, Uhispania), Ayub Timbe (Beijing Renhe, Uchina), Francis Kahata (Gor Mahia), Ovella Ochieng (Vasalund, Uswidi), Dennis Odhiambo (Sofapaka), Eric Johanna (Brommapojkarna, Uswidi), Paul Were (AFC Leopards), Cliffton Miheso (Olimpico Montijo, Ureno), Johanna Omollo (Cercle Brugge, Ubelgiji); Washambuliaji – John Avire (Sofapaka), Masoud Juma (hana klabu), Christopher Mbamba (Oddevold, Uswidi) na Michael Olunga (Kashiwa Reysol, Japan)

Tanzania (nambari 36 Afrika & 131 duniani)

Makipa – Aishi Manula (Simba, Tanzania), Metacha Mhata (Mbao, Tanzania), Aron Kalambo (Tanzania Prisons); Mabeki – Hassan Ramadan (Nkana, Zambia), Vincent Phillipo (Mbao, Tanzania), Gadiel Michael (Young Africans, Tanzania), Ally Mtoni (Lipuli, Tanzania), Mohammed Hussein (Simba, Tanzania), Kelvin Yondani (Young Africans, Tanzania), Erasto Nyoni (Simba, Tanzania), Agrey Moris (Azam, Tanzania); Viungo – Feisal Salum (Young Africans, Tanzania), Himid Mao (Petrojet, Misri), Mudathir Yahya (Azam, Tanzania), Frank Domayo (Azam, Tanzania), Farid Mussa (Tenerife, Uhispania), Yahya Zayd (Ismaily, Misri); Washambuliaji – Rashid Mandawa (BDF, Botswana), Mbwana Samatta (Genk, Ubelgiji), Thomas Ulimwengu (JS Saoura, Algeria), John Bocco (Simba, Tanzania), Abdillanie Mussa (Blackpool, Uingereza), Simon Msuva (Difaa El Jadid, Morocco).

You can share this post!

IEBC kuwahoji 10 kwa wadhifa wa afisa mkuu

Asasi za kupambana na ufisadi zatengewa fedha nyingi

adminleo