• Nairobi
  • Last Updated April 30th, 2024 5:46 PM
Vipusa wa Kahawa United wawazima wenzao wa Kangemi

Vipusa wa Kahawa United wawazima wenzao wa Kangemi

Na JOHN KIMWERE

TIMU ya wasichana ya Kahawa United iliigaragaza Kangemi Ladies kwa magoli 3-0 na kuibuka bingwa wa taji la Regional League (NRL) msimu wa 2018 kwenye mchezo uliyoandaliwa ugani Camp Toyoyo Jericho, Nairobi.

Kahawa United yambayo hutiwa makali na kocha, Joseph Wambua sasa imetwaa tiketi ya kuwania tiketi ya kufuzu kupandishwa ngazi kushiriki Ligi ya Taifa Daraja la Kwanza msimu huu.

Wasichana chini ya nahodha, Neddy Atieno watawania nafasi hiyo dhidi ya mabingwa kipute hicho katika Mkoa wa Mombasa na Mkoa wa Kati.

Kahawa United ilionyesha mchezo safi na kuzoa ushindi huo kupitia nahodha wake, Neddy Atieno aliyepiga ‘hat trick.’ Wachezaji hao walishusha mchezo wa kujiamini wakionekana kuwalemea wenzao ndani ya kipindi cha kwanza walikofunga mabao mawili.

Kahawa United na Kangemi Ladies zilicheza mchezo huo baada ya kuibuka mabingwa wa Nairobi East na Nairobi West mtawalia.

”Bila shaka nina furaha maana wachezaji wangu waliendelea kuonyesha soka safi ambapo tunakolenga kuendeleza mtindo ili kunasa tiketi ya kupandishwa ngazi,” kocha wa Kahawa United alisema.

Kocha huyo alipongeza wasichana hao kwa kuonyesha soka safi na kutinga hatua hiyo. Kadhalika wanatarajia kibarua kizito dhidi ya wapinzani wao kwa kuzingatia timu zote zitakuwa vitani kuwinda tiketi ya kufuzu kushiriki soka ya kati ya vipute vya hadhi ya juu nchini.

Kwenye kampeni za kipute cha Nairobi East Regional League (NERL) Kikosi hicho kilimaliza kidedea kwa kukusanya alama 32 bila kupoteza mchezo wowote baada ya kushinda mechi kumi na kutoka nguvu sawa mara mbili.

You can share this post!

IEBC yatuma wawakilishi katika uchaguzi wa wanachuo wa...

Nitafufua vipaji vya filamu nchini – Ruto

adminleo