Habari za Kitaifa

Moto hoteli ya kifahari Diani waongezea hofu ya majanga na ajali nchini

Na CHARLES WASONGA September 8th, 2024 1 min read

SHIRIKA la Redcross limeripoti mkasa mwingine wa moto katika mkahawa wa Diani Reef Hotel, kaunti ya Kwale.

Kwenye taarifa katika akaunti yake ya mtandao wa X, Jumapili saa kumi na mbili jioni shirika hilo hata hivyo linasema moto huo umedhibitiwa na hamna watu waliojeruhiwa.

“Maafisa wa Idara ya zima Moto katika Kaunti ya Kwale na wale wa Shirika la Msalaba Mwekundu Kenya sasa wanapambana na kisa cha moto katika Mkahawa wa Diani Reef Hotel,” KRC ikasema saa kumi na mbili na dakika tatu jioni (6.03pm).

“Moto huo hata hivyo umezimwa na hamna majeruhiwa yaliyoripoti,” shirika hilo la kutoa usaidizi nyakati za mikasa, likaongeza.

Tukio hilo linajiri wakati ambapo taifa linaomboleza vifo vya wanafunzi 21 wa Shule ya Hillside Endarasha Academy, Kieni, Nyeri Septemba 5, 2024 usiku.

Aidha, mkasa mwingine wa moto ulitokea katika Shule ya Wasichana ya Isiolo mnamo Jumamosi, Septemba 7, 2024 lakini hamna maafa yaliyotokea.