• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:15 PM
‘Tangatanga’ sasa wamtaka Uhuru kuvunja Bunge

‘Tangatanga’ sasa wamtaka Uhuru kuvunja Bunge

Na Brian Ojamaa

WABUNGE wanaoegemea mrengo wa ‘Tangatanga’ unaomuunga mkono Naibu Rais William Ruto, sasa wanamtaka Rais Uhuru Kenyatta kuvunja Bunge la Kitaifa kama alivyoshauriwa na Jaji Mkuu David Maraga.

Wabunge hao walisema jana kuwa Rais anapaswa kuzingatia Katiba kama alivyoahidi alipokula kiapo cha kuapishwa kuhudumu kwa muhula wa pili.

Walisema anapaswa kuvunja Bunge na kuitisha uchaguzi mpya.

Wabunge hao, ambao walikuwa wameandamana na Dkt Ruto kwenye hafla ya kuchangisha pesa kwa makanisa kadhaa katika eneobunge la Bumula, Kaunti ya Bungoma, walisema kuwa wako tayari kushiriki kwenye uchaguzi huo.

Mbunge wa Kuria Magharibi, Bw Mathias Robi, alisema kuwa Rais Kenyatta hana lingine ila kuvunja Bunge kama alivyoshauriwa ili kudhihirisha kwamba anatii Katiba.

“Jaji Mkuu alisema kuwa Bunge limeshindwa kupitisha Sheria kuhusu Usawa wa Jinsia. Hivyo, tunapaswa kwenda nyumbani na kushiriki upya kwenye uchaguzi. Rais hana lingine ila kufanya hivyo.”

 

You can share this post!

Madaktari waonya dhidi ya kufungua shule haraka

Mutunga ajiunga na vuguvugu jipya la kisiasa