Dondoo

Sonko ahepa kanisa waumini walipoanza kushuku anafuga majini

Na TOBBIE WEKESA August 2nd, 2024 1 min read

WAUMINI wa kanisa la hapa walimshurutisha polo kwenda kwenye altari aombewe wakishuku alikuwa amefuga majini.

“Kila mwezi anabadilisha gari. Viatu vyake pia havipatikani kwa urahisi katika masoko ya mjini hapa. Haikosi ana majini huyu mwenzetu,” waumini walisikika wakisemezana kwa sauti.

Waumini hao waliapa kumshinikiza polo aombewe na mchungaji maarufu wa kupunga mapepo.

“Lazima ufanyiwe maombi. Hakuna kazi wala biashara unayofanya lakini utajiri wako ni wa kupindukia,” jamaa alifokewa lakini akahepa.

Haijajulikana iwapo atawahi kurudi katika kanisa lake hilo au atatafuta jingine ahamie huko.