NA FARHIYA HUSSEIN
MBUNGE wa Mvita anayeondoka Abdulswamad Nassir wa Orange Democratic Movement (ODM) ndiye mshindi wa kiti cha ugavana Mombasa baada ya kumlemea mpinzani wake mkuu Hassan Omar Sarai wa United Democratic Alliance (UDA).
Matokeo ya awali kabisa yameonyesha Nassir akiwa amezoa kura 119,083 dhidi ya 98,108 za Omar.