• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 11:55 AM
Akothee adai kuwa mjamzito baada ya kuachana na mumewe mzungu

Akothee adai kuwa mjamzito baada ya kuachana na mumewe mzungu

NA MERCY KOSKEI

MWANAMUZIKI tajika Esther Akoth maarufu kwa jina la jukwaani kama Akothee amewaacha wengi na maswali baada ya kudai kuwa ni mjamzito.

Haya yanajiri siku chache baada ya tangazo lake kuwa ametengana na mumewe, Denis Schweizer aliyempa jina la utani kama ‘Omosh’.

Denis ni raia wa Uswisi.

Habari hizo zilipelekea Akothee kuwa gumzo la mitandao ya kijamii, wasanii na hata watangazaji tajika wakitoa mseto wa maoni.

Kupitia akaunti yake rasmi ya Facebook, Oktoba 8, 2023 Akothee alifichua kuwa ni mjamzito akisema kuwa ameona ni vyema kupakua habari hiyo yeye mwenyewe kabla ya bloga kuchapisha kama habari moto.

Mama huyo wa watoto watano alidai kuwa kuna bloga ambaye anafuatilia mambo yake binafsi kwa karibu, na hivyo ni vyema kuwapa mashabiki wake habari mapema.

“Vile nahisi ni kama nina ujauzito. Lakini hii mimba itakua. Omosh umetufanyaje,” aliandika.

Wafuasi wake mitandaoni walifurika kwenye safu ya maoni, wakitoa hisia tofauti kutokana na ujumbe wake, wengi wakimpongeza.

Mfuasi kwa jina Kibet Nasri alitaka kujua aliko aliyekuwa mumewe, Omosh, na kwa kejeli Akothee alimjibu kuwa yuko Pakistan.

Tabs Ke alichangia, “Akothee lunch, Akothee breakfast, Akothee dinner, tuna na kazi si haba.”

Naye Sarah Nduge aliandika, “Mtikisaji meza, tuchanganye kabisa.”

“Nilijua ni mimba ilikuwa inakusumbua…Hongera,” Let patron alimpongeza.

Hata ingawa alipotoa tangazo la kuachana na mumewe hakuweka mambo paruwanja, alisema alichukua hatua hiyo baada ya kubaini mambo fiche yaliyomshtua.

Alisema amepata nafuu kutokana na msongo wa mawazo uliomsibu.

Aliahidi kueleza baadaye sababu za kumtema Omosh.

 

  • Tags

You can share this post!

Wakazi waambukizwa ugonjwa hatari kwa kutumia maji pamoja...

Waziri Bore ashikilia makao binafsi kuokoa watoto sharti...

T L