• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 1:51 PM
Angel Di Maria ajiunga na Juventus bila ada yoyote baada ya kuondoka PSG

Angel Di Maria ajiunga na Juventus bila ada yoyote baada ya kuondoka PSG

Na MASHIRIKA

MSHAMBULIAJI mzoefu wa timu ya taifa ya Argentina, Angel di Maria, 34, amejiunga na Juventus ya Italia baada ya mkataba wake na Paris Saint-Germain (PSG) waliojivunia huduma zake kwa miaka saba nchini Ufaransa kutamatika rasmi.

Manchester United waliwahi kuweka mezani kima cha Sh8.4 bilioni kwa ajili ya Di Maria kutoka Real Madrid mnamo 2014 kabla ya kumruhusu fowadi huyo kuyoyomea PSG kwa Sh6.6 bilioni mwaka mmoja baadaye.

Akiwa PSG, Di Maria alishinda mataji matano ya Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) huku akifunga mabao 92 kutokana na mechi 295.

Di Maria anaingia katika sajili rasmi ya Juventus saa chache baada ya kiungo Paul Pogba wa Man-United kutua jijini Turin kukamilisha upya uhamisho wake hadi kambini mwa kikosi hicho

Pogba, 29, aliondoka kambini mwa Man-United mwishoni mwa msimu wa 2021-22. Anarejea Italia miaka sita baada ya Man-United kumsajili upya kutoka Juventus kwa Sh12 bilioni.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

KeNHA kuunda barabara ya Sh5.5 bilioni Thika

Ruto na Raila wazua vita kwa washirika wao

T L