Na MASHIRIKA
LIVERPOOL watakutana na Rangers ya Scotland katika hatua ya makundi ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) msimu huu huku nyota Erling Haaland akitarajiwa kumenyana na waajiri wake wa zamani baada ya Manchester City kutiwa katika zizi moja na Borussia Dortmund ya Ujerumani.
Wafalme wa Ligi Kuu ya Scotland, Celtic, wametiwa katika kundi moja na Chelsea, AC Milan na washikilizi wa taji la UEFA, Real Madrid.
Eintracht Frankfurt ambao watanogesha soka ya UEFA kwa mara ya kwanza katika historia, wamepangwa katika Kundi moja na Tottenham Hotspur.
Bayern Munich, Barcelona na Inter Milan wametiwa katika Kundi C pamoja na Viktoria Plzen kutoka Jamhuri ya Czech.
Mechi za hatua ya makundi zimeratibiwa kusakatwa kati ya Septemba 6 na Novemba 2, 2022. Fainali ya UEFA msimu huu itachezewa uwanjani Ataturk Olympic jijini Istanbul, Uturuki mnamo Juni 10, 2023.
DROO YA UEFA:
KUNDI A: Ajax, Liverpool, Napoli, Rangers
KUNDI B: Porto, Atletico Madrid, Bayer Leverkusen, Club Bruges
KUNDI C: Bayern Munich, Barcelona, Inter Milan, Viktoria Plzen
KUNDI D: Eintracht Frankfurt, Tottenham, Sporting Lisbon, Marseille
KUNDI E: AC Milan, Chelsea, RB Salzburg, Dinamo Zagreb
KUNDI F: Real Madrid, RB Leipzig, Shakhtar Donetsk, Celtic
KUNDI G: Manchester City, Sevilla, Borussia Dortmund, FC Copenhagen
KUNDI H: Paris St-Germain, Juventus, Benfica, Maccabi Haifa
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO