NA ALEX KALAMA
WENYEJI wa Tana River ambao wengi hutumia lugha ya Kipokomo wana furaha kwa sababu siku waliosubiri ya kupata Biblia kwa lugha yao, hatimaye imefika.
Spika wa bunge la Seneti Amason Kingi amewasili katika kijiji cha Idsowe, Kaunti ya Tana River kwenye hafla ya uzinduzi wa Biblia ya lugha ya Kipokomo akiwa ameandamana pamoja na seneta wa kaunti hiyo Danson Mungatana.
Kiongozi mwingine aliyeandamana na Kingi katika hafla hiyo ni seneta maalum Rafael Chimera.
Viongozi hao wamewasili katika kijiji hicho cha Idsowe kilichoko eneobunge la Garsen kwenye hafla hiyo ya uzinduzi wa Biblia iliyotafsiriwa kwa lugha ya Kipokomo na shirika la Bible Translation and Literacy.