• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Biblia ya lugha ya Kipokomo yazinduliwa

Biblia ya lugha ya Kipokomo yazinduliwa

NA ALEX KALAMA

WENYEJI wa Tana River ambao wengi hutumia lugha ya Kipokomo wana furaha kwa sababu siku waliosubiri ya kupata Biblia kwa lugha yao, hatimaye imefika.

Spika wa bunge la Seneti Amason Kingi amewasili katika kijiji cha Idsowe, Kaunti ya Tana River kwenye hafla ya uzinduzi wa Biblia ya lugha ya Kipokomo akiwa ameandamana pamoja na seneta wa kaunti hiyo Danson Mungatana.

Spika wa bunge la Seneti Amason Kingi akiwasili katika kijiji cha Idsowe, Kaunti ya Tana River kwenye hafla ya uzinduzi wa Biblia ya lugha ya Kipokomo mnamo Jumamosi, Septemba 30, 2023. PICHA | ALEX KALAMA

Kiongozi mwingine aliyeandamana na Kingi katika hafla hiyo ni seneta maalum Rafael Chimera.

Viongozi hao wamewasili katika kijiji hicho cha Idsowe kilichoko eneobunge la Garsen kwenye hafla hiyo ya uzinduzi wa Biblia iliyotafsiriwa kwa lugha ya Kipokomo na shirika la Bible Translation and Literacy.

  • Tags

You can share this post!

Kampuni za Tetra Pak na PAKPRO zashirikiana kugeuza kero ya...

Macho kwa Kipyegon na Jepchirchir mbio za barabarani...

T L