• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Club Bruges yaendeleza masaibu ya RB Leipzig kwenye UEFA

Club Bruges yaendeleza masaibu ya RB Leipzig kwenye UEFA

Na MASHIRIKA

RB Leipzig walipoteza mechi ya mfululizo kwenye kampeni za Kundi A katika Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) msimu huu baada ya kupokezwa kichapo cha 2-1 kutoka kwa Club Bruges ya Ubelgiji mnamo Jumanne usiku nchini Ujerumani.

Leipzig walioambulia nafasi ya pili kwenye kivumbi cha Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga) mnamo 2020-21, waliwekwa kifua mbele na Christopher Nkunku katika dakika ya tano kabla ya Hans Vanaken na Mats Rits kufungia Bruges mabao mawili kufikia mwisho wa kipindi cha kwanza.

Leipzig walishuka katika uwanja wao wa nyumbani kwa ajili ya mechi hiyo wakitarajiwa kujinyanyua baada ya Manchester City kuwapokeza kichapo cha 6-3 katika mchuano wa ufunguzi wa Kundi A wiki mbili zilizopita.

Washiriki hao wa Bundesliga sasa wana kibarua kizito zaidi katika mchuano ujao ikizingatiwa kwamba watakutana na Paris Saint-Germain (PSG) ya Ufaransa ugenini mnamo Oktoba 19, 2021.

PSG waliowapepeta Man-City 2-0 katika mechi nyingine ya Jumanne usiku sasa wanaselelea kileleni mwa Kundi A kwa alama nne sawa na Bruges. Man-City wanashikilia nafasi ya tatu kwa pointi tatu huku Leipzig wakivuta mkia bila alama yoyote.

  • Tags

You can share this post!

Italia na Argentina kuvaana kwenye mechi ya kuwania taji la...

Luis Suarez awaokoa Atletico Madrid kinywani mwa AC Milan...