• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 1:29 PM
Denmark kumenyana na Wales kwenye muondoano wa Euro

Denmark kumenyana na Wales kwenye muondoano wa Euro

Na MASHIRIKA

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

DENMARK watakutana sasa na Wales katika hatua ya 16-bora kwenye Euro baada ya kusajili ushindi mnono wa 4-1 dhidi ya Urusi mnamo Jumatatu usiku katika uwanja wa Parken jijini Copenhagen.

Denmark walivuna ufanisi huo siku tisa baada ya kiungo wao Christian Eriksen kuanguka uwanjani na kuzimia baada ya kupata matatizo ya moyo walipokuwa wakicheza na Finland kwenye mchuano wa ufunguzi wa Kundi B mnamo Juni 13.

Denmark walishuka dimbani wakiwa na ulazima wa kusajili ushindi kwa matumaini kwamba Ubelgiji nao wangewacharaza Finland kwenye mchuano mwingine wa Kundi B. Mabao ya Denmark yalifumwa wavuni kupitia Mikkel Damsgaard, Andreas Christensen, Yussuf Poulsen na Joakim Maehle huku Urusi wakifutiwa machozi na Artem Dzyuba.

Bao la Damsgaard lilimfanya kuwa mchezaji mchanga zaidi kuwahi kufunga bao akivalia jezi za Denmark akiwa na umri wa miaka 20 na siku 335. Denmark watavaana na Wales katika hatua ya muondoano mnamo Juni 26 jijini Amsterdam, Uholanzi.

 

  • Tags

You can share this post!

ManCity wamtia Harry Kane wa Tottenham mtegoni

Ubelgiji wapepeta Finland kirahisi na kujikatia tiketi ya...