• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Eastleigh FC yabanduliwa kutoka kipute cha Koth Biro

Eastleigh FC yabanduliwa kutoka kipute cha Koth Biro

Na JOHN KIMWERE

EASTLEIGH FC imebanduliwa kutioka kipute cha Koth Biro mwaka huu baada ya kukubali kulala kwa mabao 3-0 mbele ya Kisima FC kwenye patashika iliyochezewa ugani Umeme Ziwani, Nairobi.

Hata hivyo mchezo ulikumbwa na ghasia pale wafuasi wa Eatleigh walipoingia uwanjani baada ya mchezaji wa Kisima Kein Ojwang alipoangushwa eneo hatari na Noor Mohammed wa Eastleigh FC. Wafuasi walizua fujo wakipiga timu hiyo kupewa adhabu.

Kisima ilionyesha mechi safi na kupata ufanisi huo kupitia Lewis Shivachi aliyetikisa wavu mara mbili dakika ya 25 na 78. Nalo goli la tatu lilifunikwa kimiani na Geovanni Moses dakika ya 85.

Kwenye matokeo ya kipute hicho, Wenyeji United iliandikisha ushindi wa bao 1-0 mbele ya Kayole Youth huku Camchedu FC kutoka Shaurimoyo ilituzwa ushindi wa alama tatu kiulaini ikiwa ni ushindi wa mezani baada ya Umeme Bess kuingia mitini. Bao la Wenyeji United lilitupiwa wavuni na John Macharia kunako dakika ya 22.

Mshindi wa kipute cha mwaka huu atapokea zawadi ya Sh300, nambari mbili atatuzwa Sh100,000, nambari tatu na nne watatia mfukoni Sh 50,000 na Sh20,000 mtawalia.

You can share this post!

Uhuru aenjoi Wakenya kuhusu stima

Berita: Upshaws yazidi kumpa umaarufu katika uigizaji

T L