• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 12:30 PM
Gogo Boys imepania kumaliza kati ya tano bora

Gogo Boys imepania kumaliza kati ya tano bora

Na JOHN KIMWERE

GOGO Boys imepania kujituma kiume huku ikilenga kumaliza kati ya nafasi tano bora kwenye kampeni za Ligi ya Taifa Daraja la Kwanza muhula huu.

Kocha wake, Wilberforce Chisira amesema kuwa licha ya mtihani mgumu wanaopata kwenye mechi za kipute hicho wamekaa vizuri kutimiza azma yao. ”Sina shaka kutaja kuwa kwenye kampeni za ngarambe ya msimu huu hakuna mteremko lakini vijana wangu wanazidi kujizatiti,” alisema na kuwaomba kutolaza damu dimbani bali washiriki mechi zote kama fainali.

Kwenye matokeo ya wikendi Gogo Boys ilitoka nguvu sawa 1-1 dhidi ya Administration Police (AP). Bao hilo lilitupiwa kimiani na John Macharia. Gogo Boys inashiriki ngarambe hiyo kwa mara ya kwanza.

Klabu hiyo yenye makazi yake katika mtaa wa Kibera inajivunia huduma za wachezaji wepesi akiwamo nahodha William Oricho, Khuheib Asena, Ronald Okello, Kelvin Senya na Peter Njuguna kati ya wengine.

Klabu hiyo inakosa huduma za mchana nyavu Tyrone ‘Didis’ Kariuki aliyekuwa amejiunga na kikosi hicho kwa mkopo wa miezi sita. Hata hivyo alirejea kusakatia timu yake Rainbow FC baada ya kupigia Gogo Boys kwa miezi mitatu.

Katika jedwali ya kipute hicho Gogo Boys inashikilia nafasi ya sita kwa kutia kapuni alama 12.

You can share this post!

MUME KIGONGO: Kiasi kidogo cha pombe japo hatari, huboresha...

BIDCO imepania kumaliza nafasi ya kumi bora-FKF-PL

T L