• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 7:25 PM
Griezmann abeba Ufaransa dhidi ya Finland

Griezmann abeba Ufaransa dhidi ya Finland

Na MASHIRIKA

NYOTA Antoine Griezmann alifunga mabao mawili na kusaidia timu yake ya taifa ya Ufaransa kuwakomoa Finland 2-0 katika mechi ya Kundi D kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia za 2022 nchini Qatar.

Ushindi huo ulikuwa kitulizo kikubwa kwa kocha Didier Deschamps ambaye awali alikuwa ameshuhudia masogora wake wakiambulia sare dhidi ya Bosnia-Herzegovina na Ukraine.

Griezmann aliyerejea Atletico Madrid muhula huu baada ya kuagana na Barcelona, aliwaweka Ufaransa kifua mbele katika dakika ya 25 kabla ya kufunga bao la pili mwanzoni mwa kipindi cha pili.

Ingawa sogora huyo mwenye umri wa miaka 30 bado hajachezea Atletico mechi yoyote msimu huu, tayari amepachika wavuni mabao matatu kutokana na michuano mitatu iliyopita ya kimataifa.

Ufaransa ambao ni washikilizi wa Kombe la Dunia, sasa wanaselelea kileleni mwa Kundi D kwa alama 12 kutokana na mechi sita na wanajivunia pengo la pointi saba kati yao na Ukraine wanaokamata nafasi ya pili.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Mifuko ya supa ya Mulei ilikutwa ndani ya nyumba ya afisa...

Memphis Depay afunga mabao matatu na kuongoza Uholanzi...