• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
‘Hasla’ anatetemeshwa na umaarufu wangu – ‘Baba’

‘Hasla’ anatetemeshwa na umaarufu wangu – ‘Baba’

Na MERCY SIMIYU

KIONGOZI wa ODM, Bw Raila Odinga, amedai Naibu Rais Dkt William Ruto na washirika wake wa chama cha UDA wanaogopa umaarufu mpya ambao ODM imeanza kupata nchini.

Akihutubu jijini Nairobi jana, Bw Odinga alisema hiyo ndiyo sababu kuu ya mrengo wa Dkt Ruto kuhusisha ODM na ghasia zilizotokea Jumapili katika uwanja wa Jacaranda, eneobunge la Embakasi Mashariki.

Akimjibu Dkt Ruto, Bw Odinga alisema hakuna mfuasi wake yeyote aliyezua ghasia hizo.

Jumatatu, UDA iliwalaumu wafuasi wa Bw Odinga kuwa wahusika wakuu kwenye ghasia hizo.

“Kuna watu wanaodai kwamba wanahangaishwa wanapofanya kampeni zao. Wanasema wafuasi wa ODM waliwarushia mawe na kuvuruga mkutano wao. Ningetaka kueleza kuwa hakuna mtu yeyote aliyefanya hivyo. Tutakabiliana nao na kuwashinda kupitia wingi wa kura tutakazopata. Wameona kuna wimbi kubwa la kisiasa linalokuja ndipo wameanza kujawa na wasiwasi,” akasema.

Mara tu baada ya kisa hicho, Dkt Ruto alimlaumu Bw Odinga kwa kuwa mhusika mkuu, akisema hawatakubali vitisho kutoka kwake na washirika wake.

  • Tags

You can share this post!

Askofu ataka sheria kudhibiti fujo bungeni

Vihiga Queens, Malkia Strikers kuwania tuzo ya wanamichezo...

T L