• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 11:05 AM
Isuzu EA yaongeza mkataba na gunge Eliud Kipchoge kwa miaka miwili

Isuzu EA yaongeza mkataba na gunge Eliud Kipchoge kwa miaka miwili

Na AYUMBA AYODI

KAMPUNI ya magari ya Isuzu East Africa imeongeza ushirikiano wake na bingwa wa marathon wa Olimpiki Eliud Kipchoge kwa miaka miwili.

Mshikilizi huyo wa rekodi ya dunia mbio za kilomita 42 ya saa 2:01:39 aliandamana na mkewe Grace katika hafla ya kusaini mkataba huo mpya iliyohudhuriwa na Waziri wa Biashara na Viwanda Betty Maina mnamo Jumatano usiku.

Kipchoge alishukuru Isuzu East Africa kwa kumuamini na kuendelea kutoa usaidizi. Alitunukiwa helmeti ya Samurai.

“Helmeti ya Samurai ni heshima kubwa na ithibati ya mafanikio,” alisema Kipchoge ambaye Isuzu East Africa iliahidi kutoa msaada wa vitabu kujaza maktaba anayojenga katika eneo la Kapsisiywa katika Kaunti ya Nandi.

Ujenzi wa maktaba hiyo unakaribia kukamilika. Balozi wa Japan humu nchini Ryoichi Horie, pia alihudhuria hafla hiyo.

Kipchoge amekuwa balozi wa magari ya Isuzu D-Max tangu mwaka 2017.

TAFSIRI: GEOFFREY ANENE

You can share this post!

JUMA NAMLOLA: Wanasiasa wa Kenya waige De Klerk katika...

Buffa Otieno abwaga Tundo kuwa mwanamichezo bora nchini wa...

T L