• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 1:47 PM
Jentrix Shikangwa aanza kujenga jina TZ

Jentrix Shikangwa aanza kujenga jina TZ

NA RUTH AREGE

MSHAMBULIAJI wa Harambee Starlets, Jentrix Shikangwa, anayeipigia klabu ya Simba Queens ya Tanzania, alianza kampeni yake nchini humo kwa kucheka na wavu katika mechi ya kirafiki dhidi ya Baobao Queens siku ya Jumanne katika uwanja wa Mo Simba Arena.

Alifungia Simba bao la pekee dakika ya tano. Mechi hiyo ilikamilika kwa sare ya 1-1.

Wachezaji wanne wa Kenya, Ruth Ingotsi, kiungo Corazon Aquino na mshambuliaji Jentrix Shikangwa walianza kwenye mechi hiyo pia. Mkenya Topister Situma naye alianza akitokea benchi.

Mchezaji huyo Mkenya alirejea Kenya baada ya mkataba wake kuisha katika klabu ya Fatih Karagurumruk SK ya Uturuki. Baada ya muda mchache akiwa nchini, alipata ofa ya kujiunga na Simba.

Kikosi hicho cha Simba kiliondoka Dar es Salaam jana Alhamisi kuelekea mkoani Iringa kuweka kambi ya muda mfupi kujiandaa kwa michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Michuano hiyo itafanyika nchini Morocco mwishoni mwa mwaka huu 2022. Wakiwa Iringa, watacheza mechi za kirafiki kadhaa kama njia mojawapo ya maandalizi.

  • Tags

You can share this post!

Raila arudi mitaani kujumuika na raia

Mkenya aorodheshwa wa pili bora katika ukuzaji pamba Afrika

T L