• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 11:13 AM
KenGen kuzalisha megawati 160 kutokana na mvuke

KenGen kuzalisha megawati 160 kutokana na mvuke

Kiwanda cha kuzalisha umeme kutokana na mvuke katika eneo la Olkaria. Picha/ Maktaba

Na BERNARDINE MUTANU

KAMPUNI ya uzalishaji wa umeme nchini (KenGen) imetangaza mpango wa kuongeza megawati 160 katika mfumo wa umeme humu nchini.

Kiasi hicho cha kawi kitatiwa katika mfumo wa usambazaji wa umeme wa kitaifa kabla ya Juni 2019.

Kulingana na Meneja Mkurugenzi wa KenGen Rebecca Miano, mradi huo wa Sh17 bilioni unaendelea vyema na kufikia 2020, KenGen itakuwa na uwezo wa kuzalisha megawati 721.

Kufikia sasa, KenGen inazalisha megawati 533.8 kwa njia ya mvuke, eneo la Olkaria.

Mpango huo utaigharimu serikali Sh135 bilioni, alisema. Serikali ilizindua mpango wa kuzalisha umeme kwa njia ya mvuke katika juhudi ya kuimarisha uwepo wa kawi safi nchini.

You can share this post!

Gharama ya umeme kupanda zaidi kusiponyesha

Juhudi za Kenya kununua ndege za kijeshi zagonga mwamba

adminleo