• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 12:30 PM
Kitambi atajwa kocha bora wa mwezi KPL

Kitambi atajwa kocha bora wa mwezi KPL

Na JOHN ASHIHUNDU

Kocha wa AFC Leopards anayeondoka, Dennis Kitambi ametawazwa Kocha Bora wa Mwezi Aprili KPL.

Katika uteuzi huo uliofanywa na waandishi wa habari za michezo, Kitambi, alijinyakuliwa Sh75,000, bali na kombe kutoka kwa wadhamini wa tuzo hiyo, Fidelity Insurance.

Raia huyo wa Tanzania aliibuka mshindi baada ya kuwaongoza vijana wake kupata ushindi mara nne mwezi Machi, muda mfupi baada ya kuchuua usukani kutoka kwa Robert Matano.

“Nimeifurahia zawadi hii ambayo nimeipata wakati nikijipanga kuondoka. Nawashukuru wachezaji pamoja na wenzange tuliokuwa nao katika idara ya ukufuzni muda wote nimekuwa hapa nchini Kenya. Ufanisi wangu umetokana na msaada wa kila mtu aliyeniunga mkono.

“Naondoka japo kwa roho ngumu, lakini muda wangu wa kuondoka umefika kuambatana na mkataba wangu na Ingwe. Namtakia kocha anayechukua nafasi yangu ufanisi katika majukumu yake,” Kitambi alisema.

Kitambi ametwaa tuzo hiyo baada ya awali mshambuliaji Ezekiel Odera pia wa Ingwe kutwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa mwezi Machi.

Kitambi ataondoka nchini kesho kuelekea Bangladesh ambako atajiunga na basi wake wa zamani, Stewart Hall anayeandaa klabu ya Saif Sporting Club.

Ingwe wanashikilia nafasi ya tano jedwalini wakiwa na pointi 21 kutokana na mechi 14 wakati huu wakijiandaa kucheza na Nakumatt juma lijalo.

You can share this post!

Kipa Oluoch aikosesha Gor ushindi ugenini Rwanda

Ni udhalimu kuongeza bei ya mafuta taa, Wakenya walia

adminleo