MOSES KAPKIAI, Eldoret
UTAFITI umeonyesha kuwa kuwapa wanafunzi mapumziko kunaimarisha afya yao ya akili.
Hatua hii pia huwawezesha kuelewa vyema wanayofunzwa darasani wanaporejea baada ya likizo ikiwemo likizo fupi ya katikati mwa muhula maarufu kama ‘half term’. Kwa hivyo, sikubaliani na baadhi ya wazazi waliodai kuwa likizo fupi ya juzi haikuwa na maana yoyote na kuwa iliwasababishia usumbufu na gharama.