• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 11:34 AM
Madereva 194 kupata kazi kaunti ya Nairobi ikijiandaa kustaafisha wakongwe

Madereva 194 kupata kazi kaunti ya Nairobi ikijiandaa kustaafisha wakongwe

NA WINNIE ONYANDO

SERIKALI ya Kaunti ya Nairobi inatazamiwa kuajiri madereva 114 na waendeshaji wa mitambo 80 ili kuleta ufanisi katika kaunti na kuchukua nafasi za wafanyakazi wanaotarajiwa kustaafu.

Zaidi ya madereva 250 walioorodheshwa na waendeshaji mitambo walioteuliwa mwezi Oktoba walihudhuria mahojiano yaliyofanywa Jumanne katika uwanja wa Joe Kadenge na Bodi ya Huduma ya Umma ya Kaunti ya Jiji la Nairobi (NCCPSB).

Zaidi ya watu 15,000 walikuwa wametuma maombi ya nafasi hizi.

“Kuajiri madereva hao kutawezesha kaunti kuwa na madereva na waendeshaji mitambo walio na ujuzi. Kuna baadhi ya madereva wetu ambao wanatazamiwa kustaafu hivi karibuni, hivyo tunahitaji madereva walio na nguvu,” akasema afisa wa uchukuzi Bw Boniface Nyamu.

Kwa sasa kaunti ina waendeshaji mitambo wawili walioajiriwa huku wengine wakiwa wafanyakazi wa kawaida.

Serikali ya kaunti imeeleza kwamba watakaopewa kipaumbele katika mchakato huo ni waliowahi kuingizwa kazini wakati wa shirika la Kusimamia Jiji la Nairobi (NMS).

  • Tags

You can share this post!

Polisi wamsaka Mganda aliyeua bosi na kuhepa

Wakili amshtaki Mbunge Salasya kwa kukataa kulipa deni la...

T L