• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:08 PM
Majumba 1,437 jijini Nairobi ni hatari kuishi – NCA

Majumba 1,437 jijini Nairobi ni hatari kuishi – NCA

Na BERNARDINE MUTANU

Katika kipindi cha miaka miwili na nusu iliyopita, Mamlaka ya Kusimamia Ujenzi nchini )(NCA) imebaini kuwa majumba 1,437 ni hatari kuishi Jijini Nairobi.

Hii ni baada ya utafiti kufanywa na mamlaka hiyo alisema soroveya mkuu Moses Nyakiongora.

Tangu Janauri, familia kadhaa zimepoteza makao baada ya majumba walimokuwa wakiishi kubomoka Pipeline na Kariobangi kusini.

Kutokana na hilo, serikali inalenga kubomoa majumba yaliyothibitishwa kuwa hatari katika mitaa ya Imara Daima, Zimmerman na Huruma.

Kulingana na mhandisi wa serikali Bw Samuel Charagu majumba mawili yatabomolewa Zimmermna na sita Huruma.

Majumba mengi yaliyolengwa kwa ubomoaji huo hayajafikia kiwango cha ubora kilichowekwa.

Kulingana na utafiti huo, majumba 650 ni hatari sana na mengine 826 yanaaminika kutokuwa salama.

Majumba 4,879 yamechunguzwa na mengine 651 yanahitaji kuchunguzwa mara moja. Majumba 185 yamewekwa katika ramani eneo la Pipeline.

Kufikia sasa majumba 34 yamebomolewa na mengine 40 yalipatikana kuwa na hitilafu ambazo haziwezi kurekebishwa, kumaanisha kuwa yatabomolewa. Baadhi ya wamiliki wa majumba wamepewa muda wa makataa kurekebisha majumba yao.

Mnamo Jumamosi asubuhi, jumba lingine la orofa nne lilibomoka eneo la Ruai.

You can share this post!

Gharama ya umeme kupanda mwishoni mwa Machi

Onyo kwa wanaosafirisha mafuta chafu

adminleo