• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 3:03 PM
Marudiano kwenye raundi za tatu na nne katika Kombe la FA yafutiliwa mbali

Marudiano kwenye raundi za tatu na nne katika Kombe la FA yafutiliwa mbali

Na MASHIRIKA

MARUDIANO ya mechi za raundi za tatu na nne katika Kombe la FA yamefutiliwa mbali msimu huu ili kupunguza mrundiko wa mechi ambazo zimeahirishwa kwa sababu ya janga la corona.

Baadhi ya mechi za Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) na za daraja za chini ziliahirishwa wikendi iliyopita baada ya visa vya maambukizi mapya ya corona kuripotiwa. Katika kampeni za msimu wa 2020-21, hakuna marudiano yaliyofanyika katika raundi zote za Kombe la FA ili kupunguza presha iliyochangiwa na corona kwenye kalenda ya soka.

Mechi za raundi ya tatu kwenye Kombe la FA msimu huu zimepangiwa kufanyika kati ya Januari 7-10, 2022. Fainali itaandaliwa mnamo Mei 14 ugani Wembley.

You can share this post!

COVID-19: Mechi za EFL za Disemba 26, 2021 zaahirishwa

Kuandaliwa kwa Kombe la Dunia kila baada ya miaka miwili...

T L