Na MASHIRIKA
JUMLA ya mashabiki 1,000 watakubaliwa kuhudhuria mechi 10 tofauti katika soka ya Uingereza wikendi hii kama sehemu ya mpango wa serikali kurejesha mashabiki viwanjani baada ya janga la corona.
Maamuzi hayo ni zao la mashauriano kati ya serikali ya Uingereza na vinara wa soka ya taifa hilo (EFL) huku mashabiki zaidi wakitarajiwa kuhudhuria michuano mbalimbali kuanzia Oktoba 1, 2020.
Hakuna mashabiki wamekubaliwa kuhudhuria mchuano wowote katika soka ya Uingereza tangu Machi 2020 kwa sababu ya hofu ya msambao wa virusi vya corona.
Jumla ya mechi tatu za Daraja la Kwanza (Championship), nne za Ligi ya Daraja la Pili na tatu za Ligi ya Daraja la Tatu zimeteuliwa kwa minajili ya kufanyiwa majaribio ya kuruhusu hadi mashabiki 1,000 kuhudhuria wikendi hii (Jumamosi ya Septemba 19, 2020). Mechi hizo ni kama ifuatavyo:
Championship:
League One:
League Two:
TAFSIRI: CHRIS ADUNGO