• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 9:35 PM
Mbadi ajitosa kwa ubishi wa kurithi Gavana Awiti

Mbadi ajitosa kwa ubishi wa kurithi Gavana Awiti

Na GEORGE ODIWUOR

MWENYEKITI wa ODM John Mbadi amejiingiza katika mjadala kuhusu urithi wa Gavana wa Homa Bay Cyprian Awiti huku wanasiasa wanaokimezea kiti hicho wakijiandaa kwa kinyang’anyiro hicho 2022.

Bw Mbadi, ambaye pia ametangaza nia ya kuwania kiti hicho, anapinga pendekezo la wanasiasa hao kwamba kuwe na makubaliano kuhus

u ugavi wa nyadhifa za juu katika kaunti hiyo kuelekea uchaguzi mkuu ujao, ikiwemo ugavana.

Wanashikilia kuwa makubaliano hayo, yaliyowekwa mnamo 2013, yatumike katika uchaguzi mkuu wa 2022.

Wanasiasa hao wanasema Gavana Awiti kutoka Rachuonyo na aliyekwua Seneta marehemu Otieno Kajwang’ kutoka Suba na Mbunge Mwakilishi Bi Gladys Wanga kutoka Homa Bay mjini ni miongoni mwa waliofaidi kutokana na mwafaka huo uliofikiwa kabla ya uchaguzi mkuu wa 2013.

Wanataka mkataba huo utumiwe tena kubaini mrithi wa Gavana Awiti ambaye anakamilisha muhula wake wa pili na wa mwisho uongozini 2022.

Lakini Bw Mbadi ambaye alikuwa pamoja na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Ustawi wa Eneo la Ziwa Victoria Odoyo Owidi alifafanua kuwa wananchi wa kaunti hiyo hawakuhusishwa “wanasiasa walipokuwa wakijigawia nyadhifa.”

Akiongea katika mkutano wa kuchanga fedha katika Shule ya Upili ya Ojijo Oteko katika eneo bunge la Karachuonyo, Bw Mbadi alisema makubaliano ya 2013 yalifikiwa na wanasiasa kama watu binafsi na hayana mashiko wakati huu.

“Makubaliano hayo yalifikiwa na wanasiasa kama watu binafsi wakati huo na hayafai kutumiwa katika uwaniaji wa wadhifa wa ugavana mnamo 2022,” akasema Bw Mbadi.

Mbunge huyo wa Suba Kusini aliongeza kuwa mwafaka huo uliofikiwa katika mkutano uliofanyika katika hoteli moja jijini Nairobi unaeleweka vibaya na wanasiasa wengi katika kaunti ya Homa Bay.

“Nilihudhuria mkutano huo ambapo mwafaka huo uliwekwa. Nakumbuka kuwa washiriki walidhani kuwa wadhifa wa seneti ulikuwa na nguvu zaidi na ndipo tukakubaliana umwendee Otieno Kajwang’ kwa sababu ndiye alikuwa mwenye uzoefu mkubwa kisiasa kati yetu. Lakini sasa hayo yamepitwa na wakati,” Bw Mbadi akasema.

Kauli yake iliungwa mkono na Bw Owidi aliyedai kuwa kuna baadhi ya wanasiasa wanaoshikilia kuwa watu kutoka Rachuonyo hawafai kuwania kiti cha ugavana kwa sababu Gavana Awiti anatoka eneo hilo.

You can share this post!

Wa Iria ateua wataalamu kupiga msasa BBI

Usahihishaji wa KCSE kufanyika kwa wiki mbili

adminleo