• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 11:38 AM
‘Mchungaji’ achoma nyumba mkewe kumtomzalia watoto wa kiume

‘Mchungaji’ achoma nyumba mkewe kumtomzalia watoto wa kiume

Na MAGATI OBEBO

MWANAUME katika Kaunti ya Nyamira alichoma nyumba zake mbili kutokana na ghadhabu za kutozaliwa mtoto wa kiume na mkewe.

Alitenda ukatili huo baada ya kuchimba kaburi ili kumzika mkewe ndani na wasichana wake watatu alioapa kwamba lazima angewauwa.

Jamaa wa familia hiyo walisema Joshua Misati kwa jina la utani ‘mchungaji’ alikuwa ameishi na mkewe Rebbeca Kerubo kwa zaidi ya miaka 12 bila kujaaliwa mtoto wa kiume lakini hakuonekana kama aliyejawa na msongo wa mawazo kuhusu suala hilo.

Mkewe wa kwanza alimtoroka katika hali ya kutatanisha kufuatia ugomvi wa kila mara kuhusu kutojifungua mtoto wa kiume baada ya kujaaliwa wasichana tisa.

Hata hivyo, siku ya Jumanne usiku, mwanaume huyo kwa hasira alionekana kukosa subira na kumgeukia mkewe ambaye alifanikiwa kuponyoka kutoka mikonono mwake.

Hapo hapo alichukua kiberiti na kuchoma nyumba zake mbili, kisa kilichowashtua mno wanakijiji wa Bondeni eneo la Kebirigo, Nyamira.

Jamaa na wanafamilia walisema Bw Misati alianza ukatili wake wiki mbili zilizopita alipochimba kaburi hilo katika shamba la matunda na kuapa kuwazika mke na watoto wake wote humo.

Baadaye alilazimishwa kulifunika baada ya tambiko kufanywa na wazee ili kuwaepusha wanafamilia dhidi ya nuksi kutokana na kitendo cha Bw Misati.

Akizungumza na ‘Taifa Leo’, mkewe Bw Misati Bi Rebecca Kerubo alisimulia jinsi mumewe alivyorejea nyumbani siku hiyo kama amelewa na kuzua ugomvi naye kuhusu kukosa kujifungua mtoto wa kike.

“Alifika akigombana kuhusu chakula kisha baadaye akaanza kuuliza kwa nini nimemzalia wasichana watatu na kukosa kumzalia wa kiume,” akasema Bi Kerubo katika hali ya huzuni.

Mambo yaliharibika siku hiyo saa nne usiku alipochukua upanga na kuwafungia ndani ya nyumba kwa nia ya kuwateketeza. Waliponea kwa tundu la sindano baada ya kufanikiwa kutoroka alipokuwa akijishughulisha kuwateketeza.

“Tuliweza kutoroka wakati alipoondoka kidogo akijitayarisha kutuchoma na aliporejea alichoma nyumba zote,” akasema Bi Kerubo.

Bw Misati tayari ametoroka na anaswaka na polisi.

wa Nyamira wakiazisha msako wa kumkamata.

You can share this post!

Watalii 7,000 watarajiwa kunogesha biashara Lamu

Nitakaa na Ruto sako kwa bako, aapa Jumwa

adminleo